Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) limepokea maombi ya klabu ya Young Africans (Yanga SC) ya kutaka kufanya uchaguzi wake mkuu wa viongozi wa klabu hiyo kwa nafasi za Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na wajumbe wa kamati ya Utendaji.

TFF imeiomba klabu hiyo kufanya mkutano wake wa Uchaguzi wa viongozi baada ya kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (Rais, Wabunge na Madiwani) utakaofanyika Oktoba 25, 2015.

Hii ni kutokana na unyeti wa uchaguzi wa klabu ya Yanga yenye matawi nchini kote.

West Brom Wamnyatia Ricardo Jorge Vaz Te
Buffon Aomba Juventus Ipimwe Kupitia Man City