Msanii wa Bongo muvi nchini, Wema Isaack Sepetu amesema amejiwekea mipaka na mwanamitindo Hamisa Mobeto kwani amesema mazoea yakizidi sana na mlimbwende huyo hupelekea mushkeri.

Wema amesema hayo pindi alipoulizwa juu ya uhusiano wake na mlimbwende Hamissa Mobeto mara baada ya kuzaa na aliyewahi kuwa mpenzi wake, Diamond Platinumz na kujikuta anapunguza urafiki waliokuwa nao hapo awali.

”Hamisa ni kama Mdogo wangu, lakini kuna wakati sijui mazoea yakizidi sana kunaleta mushkeri kidogo, kwahiyo kila mtu anatakiwa kubaki kwenye mipaka yake,” amesema Wema.

Amezungumza hayo katika hafla fupi iliyoandaliwa na wasanii wa Bongo muvi ya kumpongeza mwanadada huyo kwa kujishindia tuzo za Sinema Zetu zilizoandaliwa na Azam Tv mwezi uliopita.

Aidha, Wema aliwashukuru wasanii wenzake kwa hafla hiyo na kusema ameyasikia maneno ya baadhi ya wasanii walioponda baada ya yeye kupata tuzo hizo, lakini anazichukulia kama changamoto za kimaisha.

Azam Tv ilitoa tuzo hizo usiku wa Pasaka, Aprili 1, 2018 ambapo Wema Sepetu alishinda tuzo mbili ambazo ni tuzo ya ”Best Views Choice” yaani tuzo iliyopendekezwa na mashabiki na sio majaji, na Tuzo nyingine ni Muigizaji bora wa kike.

 

 

Sababu ya Sugu kuachiwa huru yaanikwa
Maji yaua 32 baada ya ukuta wa bwawa kubomoka