Wananchi takribani 285 wa Kijiji cha Utelingolo halmashari ya wa Mji wa Njombe mkoani humo wamesema kuwa hali ya uchumi itashuka kijijini hapo kwa sababu wamekuwa wakitumia muda mwingi kupeleka na kurudisha watoto shule badala ya kufanya shughuli za kuwapatia kipato.
 
Hali hiyo imepelekea serikali ya kijiji hicho kuweka utaratibu wa kuwa na daftari maalumu la kusaini pindi unapopeleka na kuchukua mtoto katika shule husika wanayo soma.
 
‘’Sisi wanawake ndo tunateseka, kama mimi nina watoto watatu wanasoma madarasa tofauti na muda wa kutoka hivyo sasa asilimia kubwa nashinda na kazi ya kwenda kuwachukua kwa hiyo muda wa kufanya maendeleo unakua hamna,’’ amesema Mary Mlawa.
 
‘Aidha, wananchi hao wameiomba serikali kusema kitu kwani sasa hivi wanashindwa kufanya maendeleo ya kujenga nchi kwa sababu hakuna anayeruhusiwa kuchukua mtoto wa mwenzake mpaka umfuate yeye mwenyewe.
 
Kwa upande wa Chris Msigwa amesema kuwa kila kitu kimesimama na kuna hatari kubwa hapo baadae kushindwa kusomesha watoto.
 
  • Video: DC Mtwara aonya upotoshaji wa taarifa dhidi ya mauzo ya Korosho
 
  • Video: Bunge kusimamisha mshahara wa Lissu, Serikali yafunguka nyongeza mishahara
 
  • Chadema walia na mshahara wa Lissu

Shonza aipa tano 'Tetema' ya Rayvany na Diamond
Video: Makonda afanya ziara ya ukaguzi wa ujenzi wa Reli Mpya