Wakati harakati za usajili wa dirisha dogo zikiendelea katika ligi mbalimbali barani Ulaya, baadhi ya klabu zinazoshiriki kwenye ligi penda ya England, zimekamilisha usajili wa wachezaji ambao wataongeza nguvu katika duru la pili la ligi hiyo, huku wengine wakiunzwa kwa mkopo.

Usajili wa dirisha dogo ulianza rasmi juma lililopita na utafungwa rasmi Januari 31.

Dar24 tunalazimika kukuorodheshea idadi ya wachezaji waliosajiliwa na waliouzwa kutoka klabu moja kwenda nyingine, kwa orodha ya klabu shiriki katika ligi kuu ya England.

 

ARSENAL

Mpaka sasa hawajafanya usajili na hawajauza mchezaji yoyote.

 

ASTON VILLA

Klabu hii yenye maskani yake makuu Villa Park mpaka sasa imefanikiwa kumsajili kiungo Danny Drinkwater akitokea Chelsea, kwa mkopo.

Mshambuliaji wa pembeni Andre Green ni mchezaji pekee alieuzwa kwa mkopo, akisajiliwa na klabu ya Charlton Athletic inayoshiriki ligi daraja la kwanza England.

 

BOURNEMOUTH

Mpaka sasa hawajafanya usajili na hawajauza mchezaji yoyote.

 

BRIGHTON

Mpaka sasa hawajafanya usajili na hawajauza mchezaji yoyote.

 

BURNLEY

Hawajafanya usajili wa mchezaji yoyote, lakini wamewauza kwa mkopo Christian N’Guessan aliejiunga na klabu ya Oldham Athletic, Adam Phillips na Ryan Cooney wamejiunga na Morecambe.

Scott Wilson amekwenda Blyth Spartans na Will Harris amesajiliwa na klabu ya Warrington Town.

 

CHELSEA

Hawajamsajili mchezaji yoyote, lakini tayari wameshamtoa kwa mkopo kiungo Danny Drinkwater aliejiunga na Aston Villa kwa mkopo.

 

CRYSTAL PALACE

Mpaka sasa hajafanya usajili na hawajauza mchezaji yoyote.

 

EVERTON

Hawajamsajili mchezaji yoyote.

Wamewatoa kwa mkopo: Kieran Dowell (Wigan Athletic) na Callum Connolly (Fleetwood)

 

LEICESTER CITY

Mpaka sasa hajafanya usajili wala hawajauza wa mchezaji yoyote.

 

LIVERPOOL

Waliosajiliwa: Takumi Minamino (Red Bull Salzburg, ada ya usajili ni Pauni milioni 7.5), Joe Hardy akitokea Brentford.

 

Waliouzwa kwa mkopo: Herbie Kane (Hull City) na Rhian Brewster (Swansea City)

 

MANCHESTER CITY

Hawajasajili

Waliouzwa kwa mkopo: Patrick Roberts na Lukas Nmecha (Middlesbrough)

 

MANCHESTER UNITED

Hawajasajili.

Wamemuuza kwa mkopo Ethan Hamilton kwenda Bolton wanderers .

 

NEWCASTLE UNITED

Mpaka sasa hawajafanya usajili na hawajauza mchezaji yoyote.

 

NORWICH CITY

Hawajasajili.

Waliouzwa: Philip Heise amejiunga na FC Nurnberg kwa mkopo na Anthony Spyrou ameachwa kwa makubaliano maalum.

 

SHEFFIELD UNITED

Wamemsajili: Jack Rodwell (Mchezaji huru)

Hawajaacha wala kuuza mchezaji.

 

SOUTHAMPTON

Mpaka sasa hawajafanya usajili na hawajauza mchezaji yoyote.

 

TOTTENHAM

Mpaka sasa hawajafanya usajili wala hawajauza mchezaji yoyote.

 

WATFORD

Wamemsajilia: Joao Pedro (Akitokea Fluminense ya Brazil kwa makubaliano maalum)

Dimitri Foulquier amesajiliwa na klabu ya Granada kwa mkopo.

 

WEST HAM UNITED

Mpaka sasa hawajafanya usajili na hawajauza mchezaji yoyote.

 

WOLVES

Hawajasajili.

Waliondoka: Elliot Watt (Amejiunga na Carlisle kwa mkopo) na Ivan Cavaleiro (Amesajiliwa na Fulham)

Walioivaaa Young Africans waelekea Zanzibar
TMA yatangaza ongezeko la joto Dar es salaam