Serikali ya Tanzania imeahidi kuanza kuboresha maslahi ya watumishi wa uwalimu ikiwemo mishahara yao kipindi hiki mara baada ya kumaliza zoezi lililokuwa linaendelea nchi nzima la uhakiki wa wafanyakazi hewa katika sekta mbalimbali za ajira.

Hayo yamewekwa wazi na Naibu Waziri Ofisi ya Rais-TAMISEMI George Joseph kakunda Jumatano hii katika mkutano wa 10 kikao cha saba cha Bunge kinachoendelea Dodoma wakati alipokuwa akijibu swali la nyongeza kutoka kwa Mbunge wa Karagwe Innocent Bashungwa alipotaka kujua ni lini serikali itawapandishia mishahara walimu.

Utaratibu huu ambao ulikuwa umesimama kwa kipindi kifupi cha miaka kama miwili hivi kupisha uhakiki wa watumishi ambapo ni zoezi lililofanywa kwa umahiri na ueledi mkubwa, baada ya kuwa tumelikamilisha sasa tutaingia kwenye awamu ambayo ni ya kuboresha maslahi ya watumishi ikiwemo mishahara yao“, amesema Kakunda.

Kwa upande mwingine, Mhe. kakunda amewatoa hofu walimu wote ambao hawakupandishwa madaraja yao kutokea mwaka 2016 hadi 2017 na kudai katika mwaka huu wa fedha wameshafanya matayarisho wa kupandisha madaraja hayo.

Chadema yaanza kuonja machungu Songwe
LIVE: Yanayojiri Bungeni Dodoma leo Februari 7, 2018