Waliosema, “mzigo mzito mpe Mnyamwezi” ndio haohao waliokamilisha na “neno zito mpe Msukuma.” Vyote vitafika hata kwa mbinde!

Juma hili la Pasaka lilikuwa na mambo mengi na muda mchache. Wakati tunatafakari Simba alivyonywea mbele ya shamba la miwa la Kagera Sugar, huko bungeni jijini Dodoma Mbunge wa Geita vijijini, Joseph Kasheku maarufu kama ‘Msukuma’, alianzisha Ligi yake akitetea maslahi ya tasnia ya filamu nchini maarufu kama Bongo Movies kwa namna iliyozua sintofahamu.

Ni kama Msukuma alihamisha mpira wa ‘faulu’ akautenga kwenye eneo la penati na kubutua shuti kali, ‘liwalo na liwe ili mradi tupate goli la maana’. Nadhani aliona wenzake wanazunguka na mpira kulitafuta goli, wakati yeye analiona liko wazi.

Tazama hapa

Rais Putin kuwakutanisha Kim Jong Un na Rais Trump kuhusu Nyuklia
JPM awaweka mtegoni viongozi serikalini, 'Kuna watu wanatamaa sana'