Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, DKT John Pombe Magufuli, Rais mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete wameshiriki pamoja na waumini wengine kuaga mwili wa msanii mkongwe wa filamu nchini Amri Athuman maarufu kama Mzee Majuto katika viwanja vya Karimjee.

Viongozi wengine waliohudhuria shughuli hizo za kuaga ni Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Pwani, Zainab Vullu, Mufti wa Tanzania, Abubakar Zubeir, Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Musa Salum na  Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.

Video: Lijue neno la mwisho la 'King Majuto' kumwambia Muhogo Mchungu
Mfumuko wa bei wapungua kwa asilimia 3.3