Timu ya Taifa ya Wanawake (Twiga Stars) inatarajiwa kushuka dimbani siku ya jumapili kucheza dhidi ya timu ya Taifa ya Kenya (Harambee Starlets) katika uwanja wa Amani kisiwani Zanzibar ukiwa ni mchezo wa kirafiki.

Kocha mkuu wa Twiga Stars, Rogasian Kaijage amesema anaendelea vizuri na maandalizi, vijana wake wote wapo katika hali nzuri kuelekea katika mchezo huo wa kirafiki kabla ya safari ya kuelekea nchin Congo-Brazzavile.

Twiga Stars inatumia mchezo huo wa kirafiki kama sehemu ya maandalizi ya fainali za Michezo ya Afrika (All Africa Games) zinazofanyika kuanzia Septemba 4-19 nchini Congo-Brazzavile

Pique Afungiwa Michezo Minne
TFF Yavunja Ukimwa, Yaanika Ratiba Ya 2015-16