Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TF) limeviagiza vyama vya mpira wa miguu vya mikoa (FA’s) kuendesha mashindano ya ligi ya mabingwa wa mikoa kwa wanawake (Region Womens Champion League) kabla ya tarehe 31, Disemba mwaka huu.

Kila chama cha mkoa cha mpira wa miguu nchini kinapaswa kuwasilisha jina la bingwa wa mkoa mwishoni wa mwezi Disemba mwaka huu, kwa ajili ya maandalizi ya Ligi ya Taifa ya Wanawake inayotarajiwa kufanyika mwakani.

Ligi ya Taifa ya Wanawake inatarajiwa kuanza mapema mwakani baada ya kupatikana mabingwa wa mikoa 27 nchini ikijumuisha mkoa wa Dar es salaam utakaokuwa na timu tatu za Ilala, Kinondoni na Temeke.

Jumla ya timu 10 zinatarajiwa kupanda Ligi Kuu ya Wanawake Taifa baada ya timu za mikoa 27 kucheza ligi ya mabingwa na kupata timu 10 zitakazoanza kwenye ligi hiyo ya wanawake mwakani.

Advocaat: Nipo Tayari Kuitema Sunderland
Shetta Afunguka Kuhusu Tuhuma Za Kuuza Dawa Za Kulevya