Shirika la kuhudumia viwanda vidogo mkoani Njombe SIDO limesema kuwa lipo hatarini kupoteza zaidi ya mil. 100 ambazo zilikopeshwa kwa wajasiriamali, wabunifu na wamiliki wa viwanda vidogo vidogo ili kuongeza mitaji ya biashara zao kwakuwa limebaini idadi kubwa ya wakopaji walikuwa wakitoa taarifa za uongo na kugushi nyaraka.

Hayo yamesemwa na meneja wa SIDO mkoani humo, Isdori Kiyenze ambapo amesema kuwa mwaka uliopita shirika hilo lenye dhamana ya kuwainua kimitaji wajasiriamali na wamiliki wadogo wa viwanda lilitoa mikopo yenye thamani ya mil. 250 ambapo katika kiwango hicho milioni mia moja na laki nane hazijareshewa hadi sasa.

Amesema kuwa Kutokana na hali hiyo inayokwamisha mpango wa serikali wa kuwainua kiuchumi na mitaji ya wajasiriamali na wamiliki wadogo wa viwanda nchini meneja huyo ametaja hatua ambazo shirika kwa kushirikiana na mamlaka nyingine zimeanza kuchukuliwa dhidi ya wadaiwa sugu na kueleza jinsi hali hiyo inavyowakosesha haki ya kukopeshwa wahitaji wengine waaminifu.

“Tunaenda hatua kwa hatua,na itafikia mpaka kuuza zile dhamana zao na sasa yamekwishabandikwa matangazo, haya mfano hata huduma zingine usipolipa maji unakatiwa na usipolipia umeme unakatiwa na usipolipa mkopo tutachukua dhamana zako ili hela ya serikali irudi na kuendelea kuwakopesha wengine,”amesema Kiyenze

Baadhi ya wajasiriamali akiwemo Joyce Chumi na Selini John wamesema kuwa vikwazo vinavyolikumba shirika la SIDO katika ukusanyaji wa fedha hiyo imesababishwa na uwepo wa mfumo mbovu wa utoaji wa mikopo hiyo huku wakidai kwamba imekuwa ikitolewa kisiasa zaidi.

Tayari mpango wa kuanza kuuza dhamana za wadaiwa sugu unategemewa kuanza ili kunusuru upotevu wa fedha hiyo ya serikali.

Fahamu mambo muhimu kuhusu hedhi kwa mwanamke
WCB wazindua rasmi tamasha la Wasafi Festival 2019