Aliyekuwa Diwani kupitia Chama cha NCCR MAGEUZI kata ya Makere wilayani Kasulu mkoani Kigoma, Laurent Poteza, amejivua nyazifa zake zote ndani ya chama hicho na kujiunga CCM na kusema kuwa anamuunga mkono Rais Dkt. Magufuli.

Akizungunza katika baraza la Halmashauri Kuu ya wilaya ya Kasulu Mara baada ya kukabidhiwa kadi ya CCM na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Taifa, Hamphrey Polepole amesema kuwa ameamua kujiunga na CCM ili kuungana na Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuijenga nchi.

Aidha, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Taifa, Hamphrey Polepole kwa sasa yupo katika mkoa wa Kigoma na inadaiwa atakuwepo huko kwa muda wa mwezi mzima katika kujenga chama cha Mapinduzi.

Magazeti ya ndani na nje ya Tanzania leo Machi 17, 2018
Kikwete alipongeza Jeshi la Polisi, "ni hatua nzuri ya kupongezwa"