Kumpenda mtu ni kitu kingine lakini kumfanya awe na hisia kama zako juu yako ni kitu ambacho kinahitaji zaidi ya mahesabu na polojo za kumshawishi mtu huyo.

Kwa bahati mbaya, wanaume au warembo wengi wamewahi kusikia karibu maneno yote yanayotafsriwa kama ‘kuimbisha au kutongoza’, jirani zetu wa Kenya wanaita ‘Kukatia’.

Hivyo, Ni vigumu kumshawishi mtu kwa maneno yako kwa kumueleza sana kile unachokitaka kwake husasan ‘ghafla’.

Ukiacha bahati ya kuvutiana ghafla (love in first place), uhusiano wa kimapenzi unazingatia ‘theories’ za kisayansi za uhusiano na jinsi ya kuuteka ubongo na hatimaye moyo wa mtu unayetaka kuwa naye, hususan ambaye mnaweza kuwasiliana kama marafiki.

  1. Tumia Mitandao ya Kijamii, Charting

Katika karne hii karibu warembo wote wako katika mitandao ya kijamii. Kama hawako Facebook, Ello na mingine basi simu zao za kiganjani huwa na app ya Whatsap. Fahamu rafiki yako huyo unayetaka kuwa naye anapendelea mtandao gani kati ya hiyo, ukifanikisha anza kuwasiliana naye. Mtumie jumbe zinazozaa jumbe kadhaa na kuvuta usikivu wa kuwasiliana. Anza kidogo kidogo kwa kumfahamu. Usiwe na haraka ya kutaka majibu. Endelea kuwasiliana naye taratibu lakini kila unachowasiliana naye hakikisha unakiwaza na kukipanga vizuri. Kupitia jumbe zako anaweza kuanza kuvutiwa kuwasiliana na wewe kama rafiki, na hapo unaweza kuendelea kudumisha mawasiliano na kuonesha ‘busara’, kujali na mengine kama anavyoonesha kusogea. Usikurupuke.

Kwanini mitandao ya kijamii na sio jumbe za kawaida kwenye simu? Tafiti zinaonesha kuwa mitandao ya kijamii humvutia mtu kutuma jumbe na kufurahia mjadala zaidi ya jumbe za kawaida (SMS).

        2. Punguza umbali Kifkra na Kimazingira

Ukaribu katika mapenzi ni kitu kikubwa sana, anza kwanza kupunguza umbali wa kifikra kama huyo mtu yuko mbali. Tafuta kitu ambacho mnaweza kuwa na uhusiano nacho wote kwa karibu ili kiwaunganishe kifikra, iwe mtazamo, matarajio, historia zenu za maisha pamoja na mambo mengine. Hapa ni kuwa mbunifu.

Kingine ni kupunguza umbali wa kimazingira, mfanye ahisi uko karibu naye hata kama yuko nje ya nchi. Mfanye ahisi wewe uko mlango wa pili tu na utapatikana haraka endapo atahitaji kuwa karibu na wewe moja kwa moja (Physically). Onesha upo. Umbali wa kifikra na mazingira ndio sababu inayofanya uhusiano kuvunjika. Kama mko karibu unaweza kuwa unamualika ‘chakula’ na matembezi na mkawa mnaendelea kuzungumza na kuwa karibu zaidi.

          3. Mwambie Mambo yote Kuhusu Wewe lakini sio ‘kila kitu’

Wengi hupenda kuwafahamu kiundani watu ambao wako nao karibu hasa katika uhusiano wenye muelekeo wa kimapenzi. Weka vitu vyako mezani. Lakini chagua kwa makini, mwambi ahisi umemwambia yote aliyotaka kufahamu kuhusu wewe, lakini usimwambie kila kitu kwa kuwa uwazi uliopitiliza utakukosesha ‘points nyingi’. Tunza maneno yako atamani kusikia zaidi kutoka kwako.

     4. Onesha Hisia Zako Kifikra zaidi ya Kivitendo

Mfanye ugundue hisia zako kwa kukutazama na kusikiliza maelezo ya kawaida unayoongea naye. Jinsi unavyomjali na mengine. ‘Mental Emotions’ zinashika zaidi na zina nguvu kuliko ‘physical emotions’. Mfanye atumie dakika zake kadhaa kukufikiria hata kabla hujamwambia ‘Nakupenda’. Kifikra utakuwa umeshasema mengi kwake na atabaki kuwa mchambuzi na ataanza kuvutika kwako.

     5. Adimika

Siku zote kitu adimu huengezeka thamani zaidi. Jitahidi kuwa adimu kwake wakati mwingine ili umpe nafasi ya kukumiss. Hisia zako zinaongea kwa sauti kubwa zaidi kwake. Ukiwa unapatikana kila wakati kwa ajili yake atafikia hatua hatakuwa na muda mzuri wa kuvuta fikra kukukumbuka. Adimika ila usipotee.

Tafiti zinaonesha kuwa watu waliotumia formula ya kuwafuatilia wasichana kwa muda na kisha kuacha nafasi ya siku kadhaa kabla hawawajawakumbushia, hujikuta katika wakati mzuri sana hasa kama walishatengeneza ukaribu. Hiyo humfanya msichana kuwa na hamu ya kutaka kusikia.

Kumbuka kitu adimu ndicho chenye thamani zaidi. Hivyo, narudia ‘adimika’ lakini ‘usitoweke’.

Wanafunzi Walia Na Bodi Ya Mikopo, Bodi Yatoa Ufafanuzi
Nicki Minaj Ashambuliwa Baada ya Kupost Picha Hii ya Ubakaji