Imani ni kuamini juu ya mambo yatarajiwayo, katika maisha kuna nyakati mambo hutokea kwa wakati ule ule ambao unatarajia kutokea lakini kuna kuna nayakati mambo husimama au hufeli.

2019 ufanye kuwa mwaka wako wa mafanikio fikiri sahihi fanya maamuzi sahihi.

Muda mwingine jambo halitokei kwa wakati ule sio tu kwa sababu jambo hilo limefeli au limegoma kutokea ‘Hapana’ bali jambo hilo husubiri muda na wakati sahaihi kufanyika kwa jambo hilo.

Kuwa na imani kuwa na subiri, amini kuna nguvu kubwa katika subira na imani, moja ya kitabu kinachoitwa Be Rich Be Happy kilichoandikwa na Robert K Kiyosaki ambacho nilibahatika kusoma kurasa wake wa kwanza kabisa anasema ” God doesn’t create stupid people, Our Educational System does”.

Akimaanisha Mungu hajaumba watu wajinga, bali ni mifumo yetu ya elimu, ukiwaza kwa kina tafsiri hii utaelewa vizuri kabisa ujumbe ulioletwa na Bin Kiyosaki.

Ujumbe wa leo ni kwamba mwaka 2019 ukitaka kitu fanya kipaganie kwa moyo wote kisipokuwa usivunjike moyo amini wakati sahihi ukifika itakuwa vivyo hivyo utakavyo.

 

SSRA kukibeba kikokotoo cha 25% nyumba kwa nyumba
TCAA yakanusha kilio cha Masha, ‘leseni yake itafutwa...’