Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kongwa, Izengo Ngusa, amefariki dunia mara baada ya gari yake kuangukiwa na lori la mafuta.

Taarifa zinasema kuwa gari dogo alilopanda Mkurugenzi huyo, lenye namba za usajili T619 DMA aina ya Toyota Crown Athlete, liliangukiwa na lori lililokuwa limebeba mafuta.

Aidha, ajali hiyo imetokea eneo la Mbande Makaravati mkoani Dodoma, huku taarifa zikiongeza kuwa Lori hilo lililobeba mafuta limeiangukia gari ndogo na kuuwa wote walio kuwa kwenye gari hilo.

Mange Kimambi kuwaburuza mahakamani ndugu zake
Waliopotea Visiwani Pemba wapatikana wakiwa hoi