Jeshi la Polisi mkoa wa Mara linawashikilia watu zaidi ya  40, wakazi wa Kijiji cha Mikomariro wilayani Bunda kwa tuhuma za mauaji ya watu wawili sababu ikitajwa kuwa ni mgogoro wa mpaka wa shamba

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Jafari Mohamed amethibitisha kukamatwa kwa watu hao huku akiongeza kuwa Jeshi lake bado linawasaka watu wengine waliohusika na tukio la mauaji ya watu wawili wakazi wa Kijiji cha Remng’orori wilayani Serengeti.

Aidha kamanda Jafari amebainisha kuwa waliokamatwa ni wale walioshiriki yowe iliyosababisha mauaji ya watu wawili kwa kuwakata kwa mapanga kwa sababu ya ugomvi wa mipaka ya mashamba.

Hata hivyo, ameongeza kuwa chanzo cha mgogoro huo ni mpaka wa wilaya za Bunda, Serengeti na Butiama ambao unahusisha eneo la ekari 3,535 ambapo Wegesa Gikene na Nyamhanga Gembo wakazi wa Kijiji cha Remng’orori waliuawa kwa kukatwa na mapanga wakati wakiwa shambani.

JPM: Sina mpango wa kuongeza muda wa kuwa madarakani
ACT- Wazalendo wamvaa Trump