Floyd Mayweather ameeeleza kwa nini aliamua kutomchagua bondia Mwingereza, Amir Khan katika pambano la 49.

Mayweather amechagua kuzichapa na Andre Berto katika pambano litakalopigwa Jumapili.
Swali hilo limetokana na tiketi kutokuwa zimenunuliwa na haki za runinga kutogombewa hadi sasa wakati inaonekana siku zimeisha.
Khan alionekana ana nafasi ya kupigana na Mmarekani huyo mara tatu tofauti lakini aliikosa nafasi hiyo.
“Si suala la binafsi, nianchoangalia ni kazi au sema biashara. Sina matatizo na Khan lakini ndiyo niliona hivi ni sahihi kwa ajili ya biashara,” alisema Mayweather.

Arsene Wenger Atoboa Siri Ya Kutosajili
Balotelli Awapiga Dogo La Kiaina Liverpool