Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF), Jamal Malinzi amefunga kozi ya makocha ya leseni C inayotolewa na CAF, iliyowashirikisha makocha 31 kutoka mikoa mbalimbali nchini.

Akifungua kozi hiyo iliyoandaliwa na Chama cha Soka mkoa wa Dar es salaam (DRFA), Malinzi amewaomba washiriki wa kozi hiyo kwenda kutumuia ujuzi walioupata kwa kufundisha timu na vituo vya vijana vilivyopo seheu mbalimbali.

“Naimani wote hapa mlioshirki kozi hii ni watu wa mpira, ombi langu kwenu ni kwenda kufundisha mpira na sio kwenda kuviweka vyeti hivi hivi makabatini, mtusaidie kuandaa vijana kama tulivyo TFF na mipango mziuri ya kuendeleza vijana kwa ajili ya ushirki wa vijana kwenye fainali za Mataifa Afrika kwa vijaa wenye umri chini ya miaka 17 mwaka 2017 nchini Madagascar, mwaka 2019 Tanzania na baadae tuweze kushiriki fainali za Olimpiki mwama 2010 Tokyo nchini Japan.

Aidha Mwenyekiti wa DRFA Almasi Kasongo akiongea wakati wa kumkaribsisha Rais wa TFF, alisema DRFA wamejitahid kuendesha kozi hiyo yenye washiriki 31 lakini chnagamoto kubwa ni gharama za uendeshaji kwani kozi moja kama hiyo inahitaji fedha zaidi ya shilingi milioni 15 za Kitanzania jambo ambalo vyama vingine vya mikoa vinashindwa kumudu.

Navas Afichua Siri Nzito Iliyomkabili Siku Ya Mwisho
Advocaat: Nipo Tayari Kuitema Sunderland