Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi (CCM), Dkt. John Magufuli amerejesha fomu za kuomba ridhaa kuwania urais kwa tiketi ya chama hicho leo Juni 30 akiwa amedhaminiwa na wanachama takriban milini 1.02 kutoka mikoa 32.

Magufuli amerejesha fomu hizo katika ofisi za makao makuu ya CCM Dodoma nakupokelewa na Katibu Mkuu wa chama hicho dkt. Bashiru Ally pamoja na viongozi mbalimbali wa chama hicho.

Bashiru amesema leo jumanne ni siku ya mwisho kupokea fomu, na aliyechukua kwa upande wa bara ni mmoja tu ambaye ni rais Magufuli na amerejesha “fomu nimezipokea na nimethibitisha amezijaza vizuri”.

Aidha, licha ya wadhamini kutoka mikoa mbalimbali, wanachama wa UVCCM, UWT na Jumuia ya wazazi nao wamemdhamini.

Machanganuo wa wadhamini

1: Geita – 89,595

2: Arusha -22,706

3: Dar es salaam -71,491

4: Iringa- 12,542

5: Kagera- 27,245

6: Katavi- 5,071

7: Kaskazini Pemba -2,575

8: Kaskazini Unguja -1,141

9: Kigoma -30,220

10: Kilimanjaro – 23,434

11: Singda -13,452

12: Kusini pemba – 350

13: Lindi – 9,515

14: Magharibi zanzibar – 1,005

15: Manyara – 19,972

16: Njombe – 17,810

17: Pwani – 20, 603

18: Mara – 87,550

19: Morogoro – 117,450

20: Mtwara – 7,556

21: Njombe – 17, 810

22: Pwani – 20,603

23: Rukwa – 5,600

24: Ruvuma – 56,350

25: Shinyanga – 12,000

26: Simiyu- 3,693

27: Songwe- 11,744

28: Tabora- 29,489

29: Tanga- 62, 839

30: Dodoma – 44,415

Jumuia za chama

1:UWT – 66,633

2: Wazazi – 48,329

3: UVCCM – 100,360

Malawi: Mutharika aondolewa kinga, mawaziri kurudisha mali, IGP afutwa kazi
NEC yatangaza Asasi 272 zilizopita kushiriki uchaguzi Mkuu 2020