Vijana wengi wamekuwa na tamaa ya kupata fedha nyingi na kwa haraka zaidi hali ambayo inawapelekea kufanya matendo yanayohatarisha maisha ya watu wengine ikiwemo kujichukulia hatua mkononi kupoteza maisha ya watu wengine.

Vijana wengi wamekuwa wakipita njia za mkato kusaka pesa hali ambayo inawagharimu sana, kufuatia tabia hiyo kijana mmoja ambaye alikuwa ni mfanyakazi wa ndani ‘House boy’ inasemekana ameyachukua maisha ya mwajiri wake ambaye alikuwa ni mstaafu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Tunsume Sakajinga ambaye ameuawa vibaya kwa kupigwa na kitu kizito kichwani kisha kuchomwa na mkasi ambao uliachwa shingoni mwake.

Taarifa za mashuhuda wa tukio hilo ambao ni majirani wa mstaafu huyo ni kwamba kijana huyo aliamua kufanya tukio hilo la kinyama akiwa na lengo la kuchukua fedha za mafao ambazo alihisi mwajiri wake amezificha ndani kwani siku chache mara baada ya kustaafu, mama huyo amekuwa akifuatilia mafao yake.

Polisi Mkoa wa kipolisi Temeke, Emmanuel Lukula amethibitisha kutokea kwa mauaji hayo na bado taarifa za kiuchunguzi zaidi zinaendelea hasa kubaini nani hasa alihusika na mauaji hayo kwani bado haijathibitikwa kisheria kuwa kijana huyo amehusika na mauaji hayo.

Aidha kaka wa marehemu, Kisa Mwankusye amesema kuwa bado wanasubiri uchunguzi ukamilike na kukabidhiwa mwili kwa ajili ya mazishi ambayo yamepangwa kufanyika katika kijiji cha Kasanga, Rungwe mkoani Mbeya.

Majirani na watu wa karibu wa nyumba hiyo wamesema kuwa mama huyo alikuwa anaishi vizuri na kijana huyo ambaye alikuwa akisaidia kazi za nyumbani na hawajawahi kusikia malumbano ya aina yeyote kati ya wawili hao zaidi tu kijana huyo alikuwa mnyenyekevu na mwenye kutimiza majukumu yake ya hapo nyumbani.

Marehemu Tunsume Sakajinga aliishi na kijana huyo kwa muda wa miaka mitatu mpaka mauti kumkuta.

Roho ya marehemu Tunsume Sakajinga ipumzike kwa amani.

 

 

Aweso amsukuma ndani mhandisi wa maji Muleba
Video: Mnyama anayependa ngono zaidi duniani