Jumapili iliyopita rapa Kanye West alipanda kwenye Jukwaa la MTV/VMAs kupokea tuzo ya heshima ya mafanikio katika maisha yake ya muziki (Lifetime achievement award) na kuiambia dunia kuwa atagombea urais wa Marekani mwaka 2020.

Rapa huyo alitoa tangazo hilo kubwa baada ya kupokea tuzo hiyo aliyokabidhiwa na Tailor Swift, ambapo aliongea mambo mbalimbali aliyopitia katika maisha yake ikiwa ni pamoja na matukio ya kuzomewa pale alipokuwa akijaribu katika maisha mengine.

“Kama ningekuwa na mtoto katika kipindi kile ningeenda kwenda jukwaani na kunyakua Mic kutoka kwa mtu mwingine?” Alisema akikumbushia tukio alilofanya la kumpokokonya Tailor Swift Mic miaka kadhaa iliyopita kwenye tuzo hizo.

“Unajua, kesho nyakati kama hizi, itakuwa kitu kingine kabisa, tamasha fulani, kitu kama hicho. Hata ile imepita, lakini madhara yaliyokuwa na watu yamebaki. Kama mgekuwa mgeweza kuhisi hadi wakati huu, nimeamua, mwaka 2020 nitagombea urais,” alisema Kanye West.

 

Picha: Mama yake Zari afika Nyumbani kwa Diamond kumuona ‘Tiffah’
Nicki Minaj Amchana Miley Cyrus Jukwaa La MTV/VMAs