Mweusi Joh Makini amekamilisha video ya wimbo wake aliofanya na mshindi wa tuzo ya MTV/MAMA kutoka Afrika kusini, rapa AKA.

Video ya wimbo huo unaoitwa ‘Don’t’ Bother’ aliomshirikisha pia member wa kundi la Weusi, G Nako, imetayarishwa na muongozaji Justin Campos anaeheshimika zaidi Afrika kwa ubora wa video zake. Hii itakuwa collabo kubwa zaidi ya kimataifa aliyowahi kufanya Joh Makini.

Joh Makini

Hivi karibuni, Joh Makini na G Nako walienda nchini Afrika Kusini kushuti video ya wimbo huo uliotayarishwa na Nahreel ndani ya studio za The Industry.

FC Barcelona Kukosa Alves Kwa Mwezi Mzima
Picha: Lowassa Atembele Soko La Tandale Kwa Kushitukiza