Wajumbe wa Israel na wale wa Palestina wameshambuliana kwa maneno makali katika mkutano wa dharura wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ulioanyika jana kwa lengo la kuzungumzia utatuzi wa vurugu na mauaji katika ukanda wa Gaza, zinazotokana na uamuzi wa Marekani kuhalalisha Jerusalem kuwa makao makuu ya Israel.

Zaidi ya watu 58 wameripotiwa kufa kwa kufyatuliwa risasi na askari wa jeshi la Israel ambao wamepambana na waandamanaji wanaopinga uamuzi huo wa Israel na mshirika wake mkuu, Marekani.

Mkutano wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa

Katika mkutano huo wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, wajumbe kutoka Palestina walitumia maneno makali kueleza kuwa kinachofanywa na Israel dhidi ya Wapalestina ni uhalifu dhidi ya binadamu.

Pia, walilaani vikali kitendo cha Israel inayodhibiti Jerusalem kwa kutozingatia maamuzi ya Umoja wa Mataifa pamoja na kutozingatia makubaliano na sheria za kimataifa.

Hata hivyo, wajumbe wa Israel walirusha lawama zote kwa kundi la Hamas ambalo pia linadhibiti sehemu ya eneo la Gaza kwa kuwachukua mateka Waisrael na kwamba wamekuwa wakihamasisha vurugu zilizopelekea vifo hivyo.

Hii ni wiki ya sita ya maandamano makubwa yaliyozua ghasia, wapalestina wakipinga uamuzi wa Israel. Watu 58 walioripotiwa kupoteza maisha walizikwa kwa pamoja jana.

Mbowe na wenzake wakwaa kisiki Mahakamani 
Korea Kaskazini 'yaishtukia' Marekani, yadai inapanga kuifanya kama Libya