New Guinea kaunti ya Papua inatajwa kuwa ni moja ya sehemu hatari zaidi hapa duniani kwa wanawake kuishi kutokana na ukatili unaofanyika dhidi ya wanawake kwani 70% ya wanawake waishio mji huo hubakwa.

Katika mji huo wanaume wanaamini kuwa kumfanyia ukatili mwanamke ni jambo la kawaida ambalo linakubalika kwa kile walichodai kuwa ili mwanamke aweze kumtii mwanaume, ni lazima afanyiwe ukatili kwa kupigwa, kubakwa au kukatwa baadhi ya viungo vya miili yao kama vile masikio na kadhalika.

Polisi wa jiji hilo walihojiwa juu ya ukubwa wa tatizo la ukatili wa jinsia katika mji huo na kusema kuwa tatizo hilo ni kubwa sana kutokana na kesi nyingi za ukatili kuwa zimekwisharipotiwa ambazo takribani ni kesi 6000 ndani ya miezi 6 tu huku kesi nyingine nyingi zikiwa bado hazijaripotiwa.

”Kumpiga mwanamke kikatili ni moja ya tamaduni yetu hapa Papua New Guinea, huwa tunatumia kisu, bastola na kumtishia ili kumfanya aweze kutusikiliza na kufanya kile tunachotaka kama wanaume”.

”Nimewahi kumtishia mke wangu bastola na ilibakia kidogo ni mfyatulie risasi kabisa lakini bahati mbaya nilifyatua katikati ya miguu yake”. alisema mwanaume mmoja.

Wanaume hao walipoulizwa kuwa wanawapenda wake zao walijibu wanawapenda ila tu wanataka wake zao kuwasikiliza na kufanya tu kile wanachotaka wao kufanya na ni lazima wapate ruhusa kwa waume zao ndio wafanye na sio kufanya kile wanachokitaka wao.

Aidha wanawake wa mji huo wameonekana kutokuwa na furaha na wamesema ni lazima wapambane kumaliza ukatili huo unaofanyika dhidi yao kwani hawapo tayari kuona watoto wao wanaishi katika maisha hayo ya vitisho, wapo wanawake waliotoroka kabisa mji huo na kwenda kuishi sehemu nyingine kwa ajili kupata amani.

 

Video: Mke amsaliti mumewe, wafanya utekaji kwa miaka 7
Zitto aishukia serikali kuhusu Trilioni 1