Mkungu ni mti unaoweza kuota porini au wengine huupanda kwenye makazi wanayoishi. Kwa wanaoupanda nyumbani, moja ya faida wanayoipata ni kivuli chenye ubaridi asilia, mti huu wenye majani mapana kiasi, unazaa matunda maarufu kama kungu. Watu wazima hususani kinamama na watoto wanapenda kuyala matunda hayo.
Pamoja na kuzoea kula kungu , bado wengi miongoni mwao hawafahamu faida zake, Wanakula kwa kusukumwa zaidi na mazoea.
Kuna faida nyingi za kula kungu ikiwamo kusaidia mmeng’enyo wa chakula kufanyika ipasavyo tumboni kwa kuwa zimesheheni wingi wa vitamini B6, B12 na C na zina utajiri wa madini ya zinki.
Hata hivyo, baadhi ya watu wanaamini kuwa mti huu unapokuwa umepandwa au kuota wenyewe jirani au kwenye makazi ya watu, unahusianishwa na imani za kishirikina kuwa ni makazi ya pepo wabaya, dhana ambayo ni potofu. Mti huo ni kama miti mingine ya kivuli na matunda.
Majani ya mkungu yakikaushwa kivulini na kutwangwa, unga wake ukitumiwa katika uji usio mzito au maji moto unasaidia kuondoa homa mwilini, tatizo la taifodi na ini.
Pia unasaidia tatizo la vidonda vya tumbo na uzazi kwa kinamama, maumivu ya hedhi na mwasho sehemu za uzazi na hivyo kumfanya mama abaki katika hali ya furaha.

Video: Zitto amshauri Magufuli mambo 8 vita ya Corona
Maji ziwa Tanganyika yafunika Hoteli, Makazi na Kituo cha mafuta