Picha kwa hisani ya Mwananchi

Treni ya abiria imepata ajali jijini Dodoma usiku wa kuamkia leo, ikihusisha gari aina ya roli.

Kwa mujibu wa Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Patrobas Katambi, watu 29 walijeruhiwa katika ajali hiyo.

Katambi amesema kuwa Jeshi la Polisi linaendelea kumtafuta dereva wa roli lililosababisha ajali, anayesemekana kuwa alikimbia punde baada ya tukio hilo.

Jeshi la polisi limeimarisha ulinzi katika eneo hilo la ajali wakati abiria wakiendelea kuhamisha mizigo yao kutoka kwenye mabehewa yaliyoathirika na ajali hiyo.

“Bahati nzuri Kamanda wa Polisi MKoa wa Dodoma [Gilles Muroto] alikuwa hapa kwenye eneo la tukio, tuliagiza abiria wapewe ulinzi wa kutosha,” amsema DC Katambi leo asubuhi, Juni 18, 2019.

Mabehewa ya treni yanaendelea kuondolewa kwenye reli.

Video: Mbunge ataka makufuli ya TRA nchini yatupwe, Tahadhari ya ebola
LIVE: Yanayojiri bungeni jijini Dodoma leo Juni 18, 2019