Casper Nyovesto rappa kutoka Afrika ya Kusini amefunguka kuhusu muziki wao kutofika mbali na kusema kuwa wasanii wengi hawapendi kutoa ushirikiano kwenye kazi na hupenda kupata mafanikio

Ametoa kauli hiyo baada ya shabiki mmoja kutweet na kuandika mawazo yake juu ya muziki wa Nigeria na kwa jinsi unavyokuzwa na wasanii kama Davido na Wizkid baada ya Wizkid kutumbuiza kwenye tamasha  la The Ends Festival huku Davido akiwaakilisha vyema Nigeria kwenye tamasa la Hot97 summer jam Marekani wikiendi hii.

Aidha msanii huyo amesema kuwa kwenye kiwanda cha muziki Afrika ya kusini watu hawataki kushirikiana kwenye nyimbo,  wanataka kuthibitisha jinsi gani wanaweza kwenda peke yao hatuwezi kufika.

Itakuwa ni kama msanii mmoja mmoja na sio  kwa wote nimekata tamaa aliandika Cassper nyovest

 

 

Uhamiaji yatangaza mwisho matumizi ya pasipoti za zamani
Sababu yatajwa ukatili kuongezeka Njombe