Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limepitisha mswaada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria mbalimbali ikiwemo sheria ya Utumishi wa Umma, Sura ya 298  (The Public Service Act) itakayowezesha muda wa kustaafu kwa  Wahadhiri waandamizi, Maprofesa na Madaktari Bingwa kuwa miaka 60 kwa hiari na lazima miaka 65.

Hayo yamesemwa hii leo Bungeni mjini Dodoma na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masatu alipokuwa akiwasilisha mswaada huo, ambapo amesema kuwa marekebisho katika jedwali yanapendekeza kuongezwa kwa kifungu kipya cha 25A ambacho kina ainisha kuhusu umri wa kustaafu.

Amesema kuwa uzoefu umeonyesha kwamba Maprofesa na Wahadhiri waandamizi wa vyuo Vikuu vya Umma pamoja na madaktari Bingwa wa Binadamu wa Hospitali za Umma wamekuwa wakihitajika kuendelea kutoa huduma, utaalamu na uzoefu wao licha yakufikisha umri wa miaka 60.

Kwa upande wake Waziri wa Elimu Sayansi na Teknplojia, Profesa Joyce Ndalichako amesema kuwa anaunga mkono hoja  yakuongeza umri wa kustaafu kutoka miaka 60 kwa lazima hadi 65 na kutoka miaka 55 kwa hiari hadi miaka 60.

Hata hivyo, Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika mkutano wake wa 10 kikao cha 1 limepitisha mswada wa marekebisho ya sheria mbalimbali nne ambazo ni Sheria ya Ufilisi, sura ya 25, Sheria ya Bajeti, sura ya 439, Sheria ya Ardhi, sura ya 113 na Sheria ya Utumishi wa Umma, sura ya 238.

Diamond adai amekuwa
Watu wanne wafariki dunia katika machimbo ya mawe