Mario Balotelli hana nafasi katika kikosi cha Liverpool kinachofundishwa na Brendan Rodgers na katika ziara ya maandalizi ya msimu mpya, Muitalia huyo aliachwa akifanya mazoezi binafsi.

Jana wakati Manchester City ikiifumua 3-0 Chelsea katika uwanja wa Etihad, Balotelli alikuwa miongoni mwa watazamaji.

Sio kama mtazamaji wa kawaida,  klabu yake hiyo ya zamani ilimkaribisha kupitia mtandao rasmi wa Twitter.

‘Nice of @FinallyMario to pop by today, too!’ -Iliandika akaunti ya Twitter ya Man City.

The Italian striker is on the outer at Anfield, left out of their pre-season and training away from the first team

Baada ya ushindi, Straika huyo mwenye utata alionekana akimpongeza nahodha wa City, Vicent Company ambaye alifunga goli moja kati ya matatu waliyoshinda.

Wengine waliocheka na nyavu ni Sergio Aguero na Fernandinho.

Kupitia mtandao wake wa Instagram, Balotelli aliandika”Ni vizuri kushangilia ushindi na rafiki yako wa zamani”

Balotelli aliifungia City magoli 20 ndani ya miaka miwili na nusu aliyodumu Etihad na akauzwa AC Milan mwezi Januari 2013 kwa dau la paundi milioni 19.

Balotelli celebrates, in his own way, the last goal he scored all the way back on February 19 against Besiktas

Wiki ya mwisho kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili la majira ya kiangazi mwaka jana (2014), Balotelli alitua Liverpool kwa paundi milioni 16.

Baada Ya 3-0, Mourinho Ashabuliwa Mtandaoni
Murray Kidume Rogers Cup