Kocha wa Arsenal Arsene Wenger, ametoa utetezi wake juu ya kushindwa kununua mchezaji wa ndani katika dirisha la usajili lililofungwa hivi karibuni, akisema kuwa hakukuwa na mchezaji ambaye klabu ilikuwa na uhitaji naye.
Vijana hao wenye maskani yao kwenye jiji la London, walimsajili kipa Petr Cech tu kutoka Chelsea mapema kabisa wakati dirisha la usajili limefunguliwa, hali iliyojenga imani kubwa kwa mashabiki juu ya ubingwa wa EPL msimu huu, lakini hata hivyo hakuna usajili mwingine uliofanyika.
Wenger alihusishwa na tetesi za kumsajili mshambulaiji wa Real Madrid Karim Benzema lakini hata hivyo mpaka dirisha linafungwa hakuna kilichotokea.
Wenger aliwaambia waandishi: “Mwishoni, suluhisho lilikuwa si kama tulivyaka. Tuliangalia kwa makini lakini hakukuwa na suluhisho sahihi.
“Hebu angalia katika soko la wachezaji kwa sasa, utaona kwamba kuna upungufu mkubwa sana wa wachezaji. Suluhisho tulilokuwa nalo halikuwa na ushawishi kabisa.
“Habari njema kuhusu dirisha ka usajili, sasa limefungwa rasmi na tunachokiangalia kwa sasa ni kucheza mpira tu”.

Van Gaal Kumrejesha Kundini De Gea
Mayweather Atoa Sababu Za Kumkataa Amir Khan