Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Emmanuel Amunike amefanya mabadiliko kidogo kwenye kikosi chake siku chache kabla ya michuano ya AFCON 2019 kuanza nchini Misri.

Amunike amelazimika kumrejesha kikosini mlinzi wa kati wa klabu ya soka ya Azam FC, David Mwantika ili kuziba nafasi ya beki mwingine wa Azam FC Aggrey Morris.

Aggrey Morris alipata majeraha katika mchezo wa kirafiki wa Taifa Stars dhidi ya Misri uliopigwa Alhamis Juni 13, 2019 kwenye uwanja wa Borg El Arab jijini Cairo.

Aidha, mchezo huo ulimalizika kwa Tanzania kukubali kichapo cha goli 1-0 ambalo lilifungwa na Ahmed Elmohamady dakika ya 64.

Morris aliumia dakika ya 74 na nafasi yake kuchukuliwa na Ally Mtoni.

 

Mwanaume aliyejifanya mwanamke atupwa selo ya kike
Serikali kubuni njia mbadala ya kutibu ugonjwa wa Dengue