Mtu mmoja nchini Kenya mwenye umri wa miaka 35 amefikishwa mahakamani akituhumiwa kubaka mbuzi wawili wa jirani yake, na kisha kuwaua.

Tukio hilo limetokea Januari 13 mwaka huu, baada ya watu kumuona akiwaburuza mbuzi hao kutoka porini ambako anahisiwa kufanya tukio hilo, katika eneo la  Kangundo

Waendesha mashtaka wametaka mbuzi hao wapelekwe kufanyiwa vipimo ili kubaini kama kweli wamefanyiwa kitendo hicho, na kutaka mshtakiwa kupatiwa matibabu baada ya kulalamika alipigwa vibaya na polisi walipoenda kumkamata.

Kesi hiyo imehairishwa mpaka Januari 29, na mshtakiwa kupewa dhamana ya shilingi 100,000 za Kenya.

Aidha kwa sheria za Kenya zinairuhusu mahakama kumshataki mtuhumiwa kwa ukatili dhidi ya wanyama na kumhukumu kifungo cha jela kwa miaka 14.

 

Sugu: Najisikia kama Nyerere wakati wa Ukoloni au Mandela wakati wa Ukaburu
Serikali yaridhia kuboresha huduma uwanja wa ndege