Zaidi ya asilimia 30 ya maji baridi Duniani yapo katika ukanda wa Afrika, hayo yamebainishwa na Meneja wa mamlaka ya udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA) kanda ya kati, Mhandisi Norbet kayonza katika semina ya siku moja ya wakandarasi wa umeme wa manispaa ya singida.

Mhandisi Kayonza ametahadharisha kuwa licha ya mahitaji ya maji kuongezeka lakini vyanzo vya maji vinapungua kwani idadi ya watumiaji inaongezeka siku hadi siku, nakusisitiza “rasilimali ya maji duniani inapungua huo ni ukweli ambao haupingiki, lakini siyotu inapungua bali watumiaji wa maji ikiwa na maana ya idadi ya watu inaongezeka sasa ‘balance’ itatoka wapi”

Kwamujibu wa meneja huyo ameeleza kuwa uwepo wa maji baridi Duniani ni maeneo machache yaliyo bahatika huku ukanda wa Afrika mashariki ukiwa na kiwango kikubwa kwa asilimia 30 ya majiyote baridi ulimwenguni.

Hivyo amesisitiza wannchi kujitahidi kutunza vyanzo vya maji asilia kwa kuokoa kizazi kijacho, na kwa wakandarasi waliopo na wanafunzi kuendelea kuvumbua njia mbadala za kupata umeme kwa matumizi machache ya maji.

Majengo ya tume ya taifa ya uchaguzi Congo DR yateketea kwa moto
Ole wake kiongozi wa dini atakaye hubiri Siasa- Lugola